focusmedia Search This Blog

Tuesday, February 14, 2023

Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ashuhudia utiaji Saini Mikataba 26 ya Gridi Imara yenye thamani ya Shilingi Trillion 1.9, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Februari, 2023


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi mbalimbali mara baada ya kushuhudia utiaji saini wa Mikataba 26 ya Gridi Imara yenye thamani ya Shilingi Trillion 1.9. Hafla ya utiaji saini Mikataba ya kuimarisha Gridi ya Taifa na usambazaji wa umeme Vijijini imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Februari, 2023.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akishuhudia Mkurugenzi wa Shirika la Umeme nchini TANESCO Maharage Chande akiwa pamoja na Mwanasheria wa Shirika hilo Zaharani Kisilwa wakati wakitia saini Mikataba mbalimbali ya Gridi Imara na Wakandarasi mbalimbali kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Februari, 2023.
.
.
.
.
.
.
.
.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akishuhudia Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Umeme Vijijini REA Eng. Hassan Saidy pamoja na Mwanasheria wa REA Mussa Muze wakati wakitia saini Mikataba ya kupeleka Umeme maeneo mbalimbali nchini kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Februari, 2023.
Wageni mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya Utiaji Saini wa Mikataba 26 ya Gridi Imara yenye thamani ya Shilingi Trillion 1.9 Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Februari, 2023.
Wageni mbalimbali wakiwa kwenye hafla ya Utiaji Saini wa Mikataba 26 ya Gridi Imara yenye thamani ya Shilingi Trillion 1.9 Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Februari, 2023.
.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akiwa kwenye picha ya pamoja na wageni mbalimbali mara baada ya kushuhudia utiaji saini wa Mikataba 26 ya Gridi Imara yenye thamani ya Shilingi Trillion 1.9, Ikulu Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Denmark aipongeza Benki ya CRDB kwa Matokeo Mazuri ya Fedha

Balozi wa Denmark nchini, Mette Nørgaard Dissing-Spandet (wapili kushoto) katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay (wakwanza kushoto), Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori, na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakati walipomtembelea ofisini kwake kujadili uwekezaji wa DANIDA ndani ya benki hiyo na Mkakati mpya wa Miaka Mitano wa Biashara wa Benki ya CRDB wa 2023/2028.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (wakwanza kulia) akimwelezea Balozi wa Denmark nchini, Mette Nørgaard Dissing-Spandet (wapili kushoto) juu ya Mkakati mpya wa Miaka Mitano wa Biashara wa Benki ya CRDB wa 2023/2028 wakati ujumbe wa Benki hiyo ulipotembelea katika Ubalozi wa Denmark kujadili mafanikio ya uwekezaji wa DANIDA ndani ya benki hiyo. Ujumbe huo uliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay (wapili kushoto), pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (hayupo pichani), Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa (watatu kushoto), na Katibu wa Kampuni Benki ya CRDB, John Rugambo.



Na Mwandishi Wetu

Uongozi wa Benki ya CRDB kupitia Mkurugenzi Mtendaji wake, Abdulmajid Nsekela umekutana na Balozi wa Denmark nchini, Mh. Mette Nørgaard Dissing-Spandet kujadili uhusiano baina ya Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Denmark (DANIDA) na benki hiyo.

Hakuna wakati mzuri wa kujadili uhusiano huo wa kihistoria kama kipindi hiki ambacho benki hiyo kinara wa utoaji huduma za kifedha nchini, imetoka kupata faida kubwa kwa mwaka uliopita.

Ikiivunja rekodi yake yenyewe iliyoiweka kwa mwaka 2021 ya faida baada ya kodi ya takriban Sh268 bilioni na kufikia faida ya Sh353 bilioni kwa mwaka 2022.

Mafanikio hayo yanaelezwa kutokana na jitihada za makusudi za benki hiyo kukuza vyanzo vya mapato yasiyotokana na riba ambapo yaliongezeka kwa asilimia 13 mwaka hadi mwaka na kufikia kiasi cha Sh400 bilioni kutoka Sh354 bilioni.

Nsekela, akifafanua rekodi hiyo, alisema imechagiwa na ongezeko la ufanyaji miamala ya fedha hususan kupitia njia za kidijitali.

Kiujumla, wanahisa wa benki hii, DANIDA akiwa mmojawapo akishirikiana na Serikali ya Tanzania, wanaendelea kuona fahari ya kuwa sehemu ya uwekezaji wa benki inayofanya vizuri kwa kuwa wana uhakika gawio lao litaongezeka maradufu.

Balozi Dissing-Spandet akizungumza na viongozi wa Benki ya CRDB alisema amefurahishwa na matokeo mazuri ya Benki ya CRDB kwa 2022 na ni kiashiria kizuri kwa matokeo yajayo.

Historia ya DANIDA na Benki ya CRDB

Uhusiano wa DANIDA na Benki ya CRDB haujaanza leo, mizizi yake ilipandwa kupitia uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na Denmark.

Tanzania imekuwa mnufaika wa misaada ya kimaendeleo kutoka kwa Denmark kupitia DANIDA kwa miongo kadhaa iliyopita ikitekeleza miradi ya afya, uchumi, utafiti, ujasiriamali nk.

Wakati Benki ya CRDB ikijulikana kama Cooperative Rural Development Bank, ilipitia nyakati ngumu kiasi cha kushindwa kujiendesha hatua iliyopelekea Serikali kuiomba DANIDA kupitia wake Mfuko wa Uwekezaji wa Denmark (DIF) kuinasua benki hiyo.

Kuingia kwa DIF kama mwekezaji kuliweza kuleta mageuzi katika benki hiyo ambayo ilipelekea kuzaliwa upya kama Benki ya CRDB. Miaka kadhaa baadaye Benki ya CRDB ilifikia hadhi yakuweza kuorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE).

Uwekezaji wa hisa na urudishaji kwa jamii

DIF ilianza kwa kuwekeza hisa 247,014 mwaka 2002 ambazo zimeongezeka na kufikia hisa 548,067,648 mwaka 2021 ambazo ni sawa na asilimia 21 ya hisa zote za Benki ya CRDB.

Katika upande wa gawio, DIF na Serikali ya Tanzania, zilipata kiasi cha Sh247 milioni mwaka 2002 na Sh19.7 bilioni mwaka 2021.

Uhusiano huu wa aina yake baina ya DANIDA, Serikali na Benki ya CRDB umekuwa na maana kubwa katika kuifanya benki hii kuendelea kufanya vyema kila mwaka na kupata faida katika biashara yake.

Serikali ya Denmark imeendeleza ushirikiano wake na Benki ya CRDB na sasa imewekeza kupitia Mfuko wake wa Uwekezaji unaoitwa Investment Fund for Developing Countries (IFU), kwenye Kampuni tanzu ya CRDB Bank nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Kwa kuwa DANIDA ni mdau wa maendeleo nchini, inaelezwa kuwa Denmark ilikuwa miongoni mwa waasisi wa Fedha za Mfuko wa Afya wa Pamoja (HBF) mwaka 1999 na imekuwa ikiendelea kuchangia katika mfuko huo. Kwa mwaka huo pekee, ilichangia kiasi cha DKK 60 milioni.

Kupitia mchango wake katika fedha za mifuko ya afya ya pamoja kwa bara na visiwani, Danida imekuwa ikitumia fedha zake za uwekezaji kusaidia kuboresha mifumo ya afya, ubora wa huduma za afya, huduma za afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana.

Kwa mantiki hiyo, ili DIF inayoshirikiana na Serikali, iweze kuendelea kusaidia upatikanaji wa huduma za afya katika jamii zenye uhitaji mkubwa inalazimika kutenga kiasi cha gawio litokanalo na faida ya uwekezaji wake kila mwaka kwa Benki ya CRDB kufanikisha jitihada hizo.

Kwa kuwa mfuko huo na mingine bado inategemea michango kutoka kwa wadau wa maendeleo, Benki ya CRDB inabaki kuwa tegemeo la wadau wengi ambao wanachangia katika mfuko huo kupitia gawio inaloligawa kila mwaka baada ya kuwekeza hisa zao.

Ni sahihi kusema kuwa benki hiyo imekuwa ikisaidia moja kwa moja katika HBF kupitia wanahisa wake wanaopata gawio kila mwaka, kwa mantiki hiyo, ina dhima kubwa ya kuendelea kuhakikisha inakuja na mikakati bora ya kuiwezesha benki kufanya vizuri kwa mwaka huu na inayofuata na wanahisa wake kuchangia zaidi.

Kwa mwaka wa fedha 2022/23, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alisema kuwa wadau wa HBF walikubaliana kuchangia kiasi cha Sh98.1 bilioni kwa ajili ya kuboresha utoaji wa huduma za afya nchini.

“Fedha zinazoingizwa nchini kwa ajili ya kusaidia shughuli mbalimbali za afya tunapenda ziingizwe kwenye Mfuko wa Afya wa pamoja ili tuweke kushirikiana kufanya kazi pamoja na kupata matokea ya haraka kwa pamoja. Mapendekezo yetu wadau wengine wachangia kupitia mfuko huo kwani tumeona mafanikio makubwa" amefafanua Waziri Ummy Mwalimu.

Aidha Waziri Ummy Mwalimu amesema upo umuhimu kwa wadau wa maendeleo kuchanga fedha kwa pamoja na kuweka kwenye Mfuko wa Afya wa pamoja na kusema kuwa kufanya hivyo ni kuzingatia Mifumo na taratibu za Serikali za kutoa fedha kwa ajili ya Huduma za Afya nchini pamoja na kuwekeza fedha kwenye maeneo ya vipaumbele vya Serikali.

WAKULIMA RUVUMA WAINGIZA BILIONI 644 BAADA YA KUUZA KAHAWA NA KOROSHO

Shehana ya kahawa iliyokobolewa na nyingine ikiendelea kukobolewa katika kiwanda cha kukoboa kahawa cha DAE LTD mjini Mbinga



Katikati mwenye tabasamu ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas alipotembelea na kukagua kiwanda cha kukoboa Kahawa cha DAE LTD mjini Mbinga

Wakulima Ruvuma waingiza bilioni 644 kwa kahawa na korosho

Wakulima mkoani  Ruvuma waingiza zaidi ya shilingi bilioni 644 baada  kuuza mazao ya kahawa na korosho kwenye  misimu mitano mfululizo.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas amesema Mkoa wa Ruvuma kwa vipindi vya misimu ya kilimo mitano mfululizo kutoka msimu wa kilimo 2017/2018  hadi kufikia msimu 2020/2021 jumla ya kilo 77,664,927.75 za kahawazilikusanywa.

Amesema kilo hizo  ziliuzwa kwa watani wa bei sh. 4,638 na kuwapatia wakulima  wa kahawa zaidi ya shilingi bilioni  353.

Amebainisha kuwa kati ya fedha hizo,msimu wa mwaka 2016/2017  zilinunuliwa kilo  15,393.500 zilizowaingizia wakulima zaidi ya shilingi bilioni 66 na kwamba msimu wa 2017/2018 zilinunuliwa kilo 20,162,900 na kuwaingizia  wakulima zaidi ya shilingi bilioni 74.

Kwa mujibu wa Kanali Thomas katika msimu wa mwaka 2018/2019 zilinunuliwa kilo 15,675,100 zilizowaingiza  wakulima zaidi ya shilingi bilioni 64,msimu wa mwaka 2019/2022 zilinunuliwa kilo 12,676,844 zilizowaingiza wakulima zaidi ya shilingi bilioni 50  na kwamba mwaka 2020/2021  zilinunuliwa kilo 15,756,583.75 na kuwaingiza  wakulima zaidi ya shilingi bilioni 97. 

 

Monday, February 13, 2023

TANZANIA KUNUFAIKA NA BILIONI 120/- KUTOKA GEF KULINDA MAZINGIRA

Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga akifungua Warsha ya siku mbili ya Wadau na Wataalamu wa Mazingira inayolenga kuainisha vipaumbele vya miradi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayosimamiwa na GEF jijini Dodoma  Februari 13, 2023.


Wadau na Wataalamu wa Mazingira wakiwa katika Warsha inayolenga kuainisha vipaumbele vya miradi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayosimamiwa na GEF jijini Dodoma Februari 13, 2023.




Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga (kulia) akiteta Mwakilishi wa Shirika la Mazingira la Umoja wa Mataifa (UNEP) anayeshughulikia Mfuko wa GEF, Bi. Christine Haffner-Sifakis (kushoto) wakati kifungua Warsha ya siku mbili ya Wadau na Wataalamu wa Mazingira inayolenga kuainisha vipaumbele vya miradi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayosimamiwa na GEF jijini Dodoma leo Februari 13, 2023. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Switbert Mkama
Mgeni rasmi Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga (waliokaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wadau mbalimbali walioshiriki Warsha ya Warsha ya siku mbili ya Wadau na Wataalamu wa Mazingira inayolenga kuainisha vipaumbele vya miradi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayosimamiwa na GEF jijini Dodoma leo Februari 13, 2023.

TANZANIA KUNUFAIKA NA BILIONI 120/- KUTOKA GEF

 

Tanzania inatarajia kunufaika na mradi wenye thamani ya Shilingi 120 Bilioni kwa ajili ya miradi ya uhifadhi wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi kutoka Mfuko wa Mazingira wa Dunia (GEF).

 

Hayo yamesemwa leo Jumatatu (Februari 13, 2023) Jijini Dodoma na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Bi. Mary Maganga wakati akifungua Warsha ya siku mbili ya Wadau na Wataalamu wa Mazingira inayolenga kuainisha vipaumbele vya miradi ya mazingira na mabadiliko ya tabianchi inayosimamiwa na GEF.

 

Bi. Maganga amewashukuru washirika hao wa maendeleo kwa kuandaa mpango huo wa utoaji wa fedha hizo ambazo hadi sasa tayari zimekwishatolewa katika amwamu na kusema kuwa zitasaidia katika juhudi za kuimarisha uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini.

 

Aidha Bi. Maganga amewataka wadau na wataalamu hao kutumia vyema ujuzi na uzoefu walionao katika kuimarisha mapambano na changamoto za mazingira zilizopo kwa lengo la kuhakikisha maandalizi na utekelezaji wa miradi chini ya GEF- awamu ya  nane inatekelezwa kwa wakati.

 

“Tanzania ni nchi mnufaika wa miradi ya GEF ambayo inafadhiliwa kupitia mikataba mbalimbali ya kimataifa, hivyo Ofisi ya Makamu wa Rais imeona umuhimu wa kuita wadau na wataalamu kutoka wizara na taasisi za kisekta kutoka mashirika mbalimbali ili kuweka mikakati ya pamoja na kufanikisha ajenda ya mazingira,” alisema.

 

Aidha, Katibu Mkuu Maganga ametoa wito kwa wataalamu hao kuhakikisha wanafanya maandalizi ya haraka ya kuainisha maeneo ya kipaumbele ya miradi ya washirika wa maendeleo ili kuanza katika uliowekwa na kuikamilisha kwa wakati.

 

Kwa upande wake Mratibu wa GEF – Kanda ya Afrika Bw. Ibrahima Sow alisema kuwa Tanzania imetengewa mgao huo wa fedha za mzungumzo wa nane katika maeneo matatu ya mradi kwa kipindi cha miaka minne ijayo.

 

Alitaja maeneo hayo kuwa ni mradi wa usimamizi katika Maziwa Makuu na Mabonde ya Maji, fedha za kujenga uwezo kwa wataalamu wa miradi pamoja na usimamizi wa miradi katika nchi zinazoendelea. 

 

Naye Mkurugenzi wa Mazingira Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Andrew Komba alisema kuwa katika eneo la kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, Serikali imeendelea kushirikiana na wadau mbalimbali na kuhimiza na kuhamasisha utunzaji wa mazingira.

 

Alisema kuwa mabadiliko ya tabianchi ni miongoni mwa matokeo ya kuongezeka kwa gesijoto duniani sambamba na uharibifu wa uoto asili na bioanuai, hivyo Serikali imeanzisha kampeni za upandaji miti ili kuhakikisha nchi inakabiliana na athari hizo.

 

Naye Mwenyekiti wa Jukwaa la Wadau wa Mazingira Nchini Bw. Tumaini Marijani aliipongeza Serikali kwa namna inavyoratibu masuala ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini.

 

Tumaini, pamoja na kuhamisha wadau wakiwemo taasisi binafsi kushiriki shughuli za mazingira,  pia aliwataka watalaamu na wadau hao kushiriki zoezi la upandaji wa miti ili kuunga mkono juhudi za Serikali katika uhifadhi na usimamizi wa mazingira.

  

Warsha hiyo inatoa fursa kwa Tanzania na wadau wa ndani na nje ya nchi kujadili na kupeana uzoefu katika mafanikio na namna ya kutatua changamoto zilizopo na zinazoweza kutokea katika miradi iliyopita na inayoendelea kutekelezwa.

 

Wednesday, February 8, 2023

RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI DK.HUSSEIN ALI MWINYI AMEKUTANA NA MKURUGENZI MKAZI WA BENKI YA DUNIA NCHINI TANZANIA NATHAN BELETE NA UJUMBE WAKE








 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi amekutana na Mkurugenzi mkazi wa Benki ya Dunia Nchini Tanzania Nathan Belete na ujumbe wake. 

 

Dk. Mwinyi ameipongeza Benki hiyo inavyoiunga mkono Zanzibar katika Miradi mikubwa hasa mradi wa Umeme, Afya na Elimu.

 

Rais Dk.Mwinyi ameiomba benki ya Dunia kusaidia katika Elimu ya Ufundi hasa kutokana na Wanafunzi wengi kutopata nafasi ya vyuo vikuu.

 

Dk.Mwinyi amemueleza Mkurugenzi huyo sera ya uchumi wa Zanzibar ni Uchumi wa Buluu, Utalii na Bandari, pia katika suala la miundombinu Serikali imekamilisha ujenzi wa uwanja wa ndege wa Kimataifa Unguja na sasa nguvu zimeelekezwa kujenga uwanja mpya wa ndege wa Kimataifa wa Pemba. 

 

Pia, Dk.Mwinyi aliitaka benki hiyo kuharakisha mchakato wa upatikanaji wa fedha za miradi ya maendeleo

 08 Februari 2023

 

📍 Ikulu ,Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi atembelewa na Madaktari wapya kutoka China wakiongozwa na Balozi mdogo wa China, Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng







 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema ujio wa madaktari bingwa kutoka China ni fursa adhimu kuimarisha sekta ya Afya Zanzibar.
 
Dk. Mwinyi amesema timu ya madaktari bingwa kutoka China imewasili Zanzibar kuongeza nguvu katika sekta ya Afya kwa kutoa wataalamu mbalimbali wakiwemo Madaktari bingwa wa operesheni bila kupasua, magonjwa ya kina mama, magonjwa ya meno, magonjwa ya koo, macho na masikio pamoja na kutoa vifaa vya kisasa.
 
 
Madaktari hao watafanya kazi za kitabibu katika hospitali za Mikoa ya Unguja na Pemba ikiwemo Hospitali ya Mnazi Mmoja, Abdalla Mzee, Chake Chake na Kivunge.
 
Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo alipotembelewa Ikulu Zanzibar na Madaktari wapya kutoka China 
 
Ujumbe huo wa Madaktari umeongozwa na Balozi mdogo wa China, Zanzibar Mhe. Zhang Zhisheng
 
 
📅 08 Februari 2023
 
📍 Ikulu ,Zanzibar.