focusmedia Search This Blog

Monday, October 31, 2016

HOTUBA YA RAIS MAGUFULI NA RAIS KENYATTA KENYA

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesema kuwa Kenya ndio mshirika nambari moja wa Tanzania katika uwekezaji na biashara barani Afrika.
Akizungumza katika ikulu ya rais jijini Nairobi mda mfupi baada ya kuwasili nchini Kenya,Rais Magufuli amesisitiza kuwa hakuna taifa jingine ambalo limewekeza nchini mwake kama Kenya.
Amesema kuwa kulingana na rekodi za uwekezaji nchini Tanzania kuna takriban kampuni 529 nchini humo kutoka Kenya ambazo zinaingiza takriban dola bilioni 1.7 kila mwaka huku takriban Watanzania 57,260 wakiwa wameajiriwa.
Rais huyo vilevile ametoa wito kwa Wakenya wanaotaka kuwekeza nchini Tanzania kuharakisha hatua hiyo.
Aidha ameongezea kuwa amekuwa akiwasiliana na rais Uhuru Kenyatta mara kwa mara na kiwakosoa wale wanaodhani kwamba uhusiano wake na rais wa Kenya una utata.

MAGUFULI: KENYA NI MSHIRIKA WETU MKUBWA KIBIASHARA AFRIKA


RAIS wa Tanzania John Pombe Magufuli amesema kuwa Kenya ndio mshirika nambari moja wa Tanzania katika uwekezaji na biashara barani Afrika.
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amesema kuwa Kenya ndio mshirika nambari moja wa Tanzania katika uwekezaji na biashara barani Afrika.
Akizungumza katika ikulu ya rais jijini Nairobi mda mfupi baada ya kuwasili nchini Kenya,Rais Magufuli amesisitiza kuwa hakuna taifa jingine ambalo limewekeza nchini mwake kama Kenya.
Amesema kuwa kulingana na rekodi za uwekezaji nchini Tanzania kuna takriban kampuni 529 nchini humo kutoka Kenya ambazo zinaingiza takriban dola bilioni 1.7 kila mwaka huku takriban Watanzania 57,260 wakiwa wameajiriwa.
Rais huyo vilevile ametoa wito kwa Wakenya wanaotaka kuwekeza nchini Tanzania kuharakisha hatua hiyo.
Aidha ameongezea kuwa amekuwa akiwasiliana na rais Uhuru Kenyatta mara kwa mara na kiwakosoa wale wanaodhani kwamba uhusiano wake na rais wa Kenya una utata.Ikulu Nchini Tanzania Imetoa Taarifa kwa vyombo vya habari nchini.

Friday, October 28, 2016

VIJANA WAAMUA KUIJENGA TANZANIA,MatokeoChanyA

VIJANA WAAMUA KUIJENGA TANZANIA,MatokeoChanyA+

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA BALOZI WA HESHIMA WA TANZANIA NCHINI FINLAND

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewakaribisha wawekezaji kutoka nchi ya Finland kuja kuwekeza katika sekta mbalimbali nchini ikiwemo ya nishati katika kipindi hiki wakati ambapo taifa la Tanzania linaelekea katika uchumi wa viwanda.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Heshima wa Tanzania nchini Finland Vesa Viitaniem
 
Makamu wa Rais amesema kuwa mkakati wa sasa wa Serikali ni kuhakikisha taifa linajitosheleza ipasavyo katika nishati ya umeme hatua ambayo itasaidia wawekezaji wengi kutoka mataifa mbalimbali Duniani kuja kuwekeza nchini kutokana na nchi kuwa na umeme wa kutosha na wa uhakika utakaotumika katika viwanda vitakavyojengwa katika maeneo mbalimbali Nchini.
Makamu wa Rais pia ameishukuru Serikali ya Finland kwa kuendelea kuisaidia Tanzania katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Elimu na kuwezesha makundi mbalimbali ya kijamii hapa nchini ikiwemo ya wanawake,yatima na vijana.
 
Makamu wa Rais amemweleza Balozi huyo kuwa kwa sasa jitihada kubwa za Serikali ya awamu ya Tano zimeelekezwa katika uimarishaji wa miundombinu ikiwemo reli, bandari na barabara ili kurahisisha usafiri na usafirishaji wa bidhaa mbalimbali kote Nchini.

Kwa upande wake, Balozi wa Heshima wa Tanzania nchini Finland Vesa Viitaniem amemhakikishia Makamu wa Rais kuwa nchi ya Finland itaendelea kushirikiana na Serikali katika kusaidia uimarishaji wa huduma bora kwa wananchi ikiwemo kuwezesha wajasiriamali ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.
 
Mahusiano mazuri kati ya Tanzania na Finland yamewezesha Watanzania zaidi ya 500 kuishi nchini humo kwa ajili ya shughuli mbalimbali ikiwemo za kimasomo.
Balozi wa Heshima wa Tanzania nchini Finland Vesa Viitaniem aliongozana na Mke wa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Mama Anna Mkapa.


Thursday, October 6, 2016

#MatokeochanyA MADAWATI


Katika kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli alilolitoa Machi 16,2016 wakati anawaapisha wakuu wa mikoa kuhusu utekelezaji wa elimu bila malipo,Rais aliwataka wakuu hao wa mikoa kuhakikisha wanasimamia upatikanaji wa madawati ifikapo Juni mwaka huu. Mkoa wa Mtwara chini ya uongozi wa mkuu wa mkoa huo Mheshimiwa Halima Dendego umedhamiria kukamilisha suala la madawati ifikapo Mei 2016 kwa Halmashauri zote tisa zinazounda mkoa huo Masasi mji ikiwemo kutumia njia mbalimbali ili wanafunzi wote wakae kwenye madawati. Katika kikao kilichoitishwa Februari, mwaka huu na mkuu wa mkoa wa Mtwara baada ya kubaini changamoto hizo, wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa wilaya waliagizwa kuhakikisha wanashughulikia changamoto hizo hasa uhaba wa madawati ambapo kwa ujumla mkoa wa Mtwara una upungufu wa madawati 35,406. Kwa upande wa Halmashauri ya mji wa Masasi tayari mchakato wa upatikanaji wa madawati hayo umeanza kwa kutumia rasilimali zilizopo pamoja na mapato ya ndani sambamba na kushirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo zikiwemo taasisi za serikali,taasisi binafsi za kifedha,wafanyabiashara pamoja na wananchi wote kwa ujumla kwa lengo la kuhakikisha kuwa ifikapo Mei 2016 watoto wote wanaokaa chini wa madawati.


   




#MatokeochanyA ARUSHA NI MJI WA KITALII


Mkoa wa Arusha

Mkoa wa Arusha

Mlima Ol Doinyo Lengai karibu na kijiji cha Ngare Sero, Mkoa wa Arusha.
Mlima Ol Doinyo Lengai karibu na kijiji cha Ngare Sero, Mkoa wa Arusha.

Mahali pa Mkoa wa Arusha katika Tanzania
Mahali pa Mkoa wa Arusha katika Tanzania
Anwani ya kijiografia: 3°0′S 36°0′E
6
 - Mkuu wa Mkoa
Isidori Shirima
 - Mkoa
86,100 km²
 - Maji
2,460 km² 
Idadi ya wakazi (2002)
 -
1,288,088
Tovuti: http://www.arusha.go.tz/
Mkoa wa Arusha ni moja kati ya mikoa 30 ya Tanzania. Imepakana na Kenya upande wa kaskazini. Mikoa ya jirani ni kufuatana na mwendo wa saa: Kilimanjaro, Manyara, Shinyanga na Mara. Mkoa wa Arusha ni Mkoa wa pili kwa Utajiri nchini Tanzania.
Wilaya zake ni Monduli, Longido, Meru, Arusha Vijijini, Arusha Mjini,Ngorongoro na Karatu. Makao makuu yapo Arusha mjini.
Eneo lake ni km za mraba 86,100 zikiwemo km² 2,460 za maji. Kati ya milima yake Oldoinyo Lengai (2,878 m) bado ni volkeno
hai, na mlima Meru ni volkeno ya kulala tangu mw. 1910. Mvua hunyesha
kati ya millimita 1,800 mm kwa mwaka mlimani Arusha hadi 508 mm kwa
mwaka katika maeneo makavu.
Mkoa wa Arusha ndio kitovu cha utalii Tanzania Bara. Barabara ya lami Dar Es Salaam-Nairobi inavuka eneo lake. Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Kilimanjaro wahudumia miji ya Arusha na Moshi. Kuna mbuga za taifa na hifadhi za wanyamapori Ngorongoro, Serengeti, Olduvai, Arusha, Tarangire na Ziwa Manyara. Hifadhi ya Mlima Kilimajaro iko karibu.
Arusha hulimwa kahawa, nafaka, pareto, katani, pamba, alizeti.
Fosfati inachimbuliwa Minjingu Mkoani Arusha, na takribani tani 48,000
kwa mwaka hutumiwa katika uzalishaji wa mbolea.
Kati ya wakazi wa mkoa kiasili ndio Waarusha, Wameru, Wairaqw na Wamassai.

Majimbo ya Bunge

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo: